Wakati Wa Mungu – Paul Clement & Guardian Angel

[Verse One]
Wakati wa Mungu nikama tsunami ya maji
ukuta hauezi kuzuia
lazima utabomoka.

Wakati wa Mungu
nikama upepo mkali
mlango hauezi kuzuia
lazima utafunguka
Wakati wa Mungu

humpata kila mtu
we kuwa na subira
andika haya kwenye shajara
Wakati wa Mungu ukikujilia

mazingira si kitu yapinge
Wakati wa Mungu ukikujilia
mwanadamu ni nani apinge.

{Chorus}
Usichoke
ngoja x 6
ukujilie
Wewe subiri tu

[Verse Two]
Yo nilisoma na ma guys na washapata ma kazi
Mwanafu anapata fursa ya kula cha mkufuu
Mimi bado nauliza kama nitawai pata nafuu
ama kweli talanta itafanya nile na wakuu.

Wakati waa Mungu je utawai nifikia
baraka zangu niweze kuzipokea?
Wakati wa Mungu kweli utakufikia
baraka zako ueze kuzipokea
nimechoka kungoja ….

{Chorus}
Usichoke
ngoja x 6
ukujilie
Wewe subiri tu

{Bridge}
Shida juani natamani kivulini,
nipate amani ooh..
Jua Mungu ni mti wenye kivuli kizuri
Ni mti wenye uzima na kweli.

Wakati wa Mungu hufanya njia janguwani
mito ya maji jangwani
wakati wake hauna upinzani.
Kumbe wakati wa Mungu

huwafanya adui zangu kuwa rafiki zangu
kila kitu huwa raisi ata vilivyo shindikana

{Chorus}
Usichoke
ngoja x 6
ukujilie
Wewe subiri tu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *