USIFURAHI JUU YANGU Lyrics by Upendo Nkone

Usifurahi juu yangu eeeh adui yangu
Niangukapo mimi nitasimama tena

Kumbuka niwapo gizani bwana ni nuru yangu
Hawezi kuniacha bwana mimi niangamie ×2

Si vyema kunisema vibaya nipatapo tatizo
Shetani wampa nafasi ndani ya moyo wako
Kumbuka kwa maombi yako nitasimama tena
Na utapata baraka kutoka kwake mungu ×2

Maana heri mtu yule ambaye kinywa chake
Ni kuwabariki wenzake na kiwaombea
Maana maneno mabaya huchafua moyo

Ukiwekwa mbali na mungu ni vyema uwe safi
Ukiona niko kwenye shida niombee
Ndoa yangu imevunjika wewe niombee

Nikifukuzwa kazini ndugu niombee
Magonjwa yananiandamaa niombee
Biashara haina faida niombee

Nikikawia kupata mtoto niombee
Nimekuwa mtoto yatima niombee
Ata nijapo kuwa mjane niombee

Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa ×4

1 thought on “USIFURAHI JUU YANGU Lyrics by Upendo Nkone

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *